Skip to main content

DAWA ZA KUEPUKA KAMA UNA KISUKARI

Dawa gani nisitumie kama nina Kisukari?
picha ya mfamasia akikagua dawa

Katika sayansi ya dawa kuna kitu kinaitwa muingiliano (drug interaction), hii inaweza kuwa muingiliano kati ya dawa na dawa, muingiliano kati ya dawa na ugonjwa, au muingiliano kati ya dawa na chakula. 

Katika makala hii tutaangazia muingiliano wa dawa na ugonjwa wa kisukari pia muingiliano wa baadhi ya dawa na dawa za kisukari, kuna dawa ambazo zinaweza kusababisha sukari ya mwili kupanda, au dawa ambazo zinaweza kuzuia dawa zako za kisukari zisifanye kazi yake vizuri. 

Kisukari ni nini?
picha ya kipimo cha kisukari


Kisukari ni hali ambayo husababisha kiwango cha sukari katika damu kuwa juu isivyo kawaida. Kulingana na sababu zinazoweza kusababisha hali hii, kuna aina mbalimbali za kisukari:

Kisukari Aina ya 1 (Type 1 Diabetes)

Hii ni hali ambapo mwili hauwezi kuzalisha insulini kabisa. Hii ni kwa sababu seli za kongosho (pancreas) zinashambuliwa na mfumo wa kinga wa mwili na kuharibiwa. Hali hii inaweza kuwa ya kurithi na mara nyingi huanza utotoni au ujana, lakini inaweza kutokea kwa watu wa umri wowote. 

Kisukari Aina ya 2 (Type 2 Diabetes)

Hii ni hali ambapo mwili unashindwa kutumia vizuri insulini (insulin resistance) au hauzalishi insulini ya kutosha. Aina hii ya kisukari mara nyingi huhusishwa na maisha ya mtindo duni, uzito wa kupindukia na historia ya familia. 

Kisukari Cha Mimba (Gestational Diabetes) 

Hii ni hali ambapo mjamzito anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu, hii husababishwa na mwili wa mjamzito kushindwa kutumia insulini vizuri. Mara nyingi hali hii huanza kutokea kati ya wiki ya 24 na 28 ya ujauzito. 

Dalili za Kisukari

  • Kiu kali
  • Kukojoa mara kwa mara
  • Njaa isiyoisha
  • Uchovu mwingi
  • Kupungua uzito bila sababu
  • Vidonda vinavyopona polepole
  • Kuona ukungu

Dawa za kuepuka ikiwa una kisukari

STEROIDS 
Picha ya dawa za corticosteroids ambazo zinaweza kuathiri viwango vya sukari kwa wenye kisukari

Steroids hasa zile zinazojulikana kama "corticosteroid" (prednisolone, dexamethasone na hydrocortisone), zinapotumiwa kwa muda mrefu au kwa dozi kubwa zina athiri jinsi mwili unavyo dhibiti kiwango cha sukari kwenye damu. Hii inaweza kuwa na athari kubwa kwa watu wenye kisukari au ambao wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu. 

Jinsi steroids zinavyoweza kuathiri viwango vya sukari

Huongeza kiwango cha sukari kwenye damu: 

Pale kiwango cha sukari kwenye damu kinapokuwa juu, kongosho inatoa insulini, insulini itaenda kwenye ini na kutoa ishara ini liache kumwaga sukari kuingia kwenye mfumo wa damu, badala yake inaituma sukari kwenye seli moja kwa moja. 

Dawa za steroids husababisha ini lisipokee taarifa ya insulini (aidha ni insulini iliyozalishwa na mwili au insulini inayotumika kama dawa na mgonjwa wa kisukari), na ini huendelea kumwaga sukari kwenye mfumo wa damu. 

Matumizi ya steroids yanaweza yasihepukike kwa baadhi ya magonjwa, ndio maana ni muhimu kutoa taarifa kamili kwa daktari wako, ili aweze kufanya mabadiliko aidha kwenye dozi za steroids ama dawa zako za sukari. 

Huongeza hamu ya kula

Steroids zinaweza kuongeza hamu yako ya chakula, hii inaweza kuchangia ongezeko la viwango vya sukari kwenye damu. 

Hubadilisha usambazaji wa mafuta

Steroids hubadilisha jinsi mwili unavyo sambaza na kuhifadhi mafuta, zinaweza kusababisha mkusanyiko wa mafuta katika baadhi ya maeneo ya mwili kama vile uso, shingo na tumbo. Hali hii inajulikana kama "Cushingoid appearance"


BETA BLOCKERS

Dawa hizi hutumika kudhibiti shinikizo la damu (hypertension), mfano propranolol, atenolol na metoprol. Kwa wagonjwa wenye magonjwa yote mawili (Kisukari na Shinikizo la Damu) matumizi ya beta blockers yanaweza kuleta shida kwenye upande wa Kisukari. 

picha ya beta blockers

Jinsi Beta Blockers zinavyoweza kuathiri matibabu ya kisukari  

Zinaongeza hatari ya Sukari ya kiwango cha chini (Hypogylcemia)

Kwa mgonjwa wa Kisukari anayetumia dawa kama insulini au glimepiride kwa pamoja na beta blocker kama propranolol, anaweza asihisi mapema dalili za  sukari ya chini hivyo kusababisha hypoglycemia kali. 
Dalili kama vile mapigo ya moyo kwenda kasi, mitetemo, na wasiwasi hufichwa na matumizi ya beta blockers.

Pia beta blockers hudhoofisha uwezo wa ini kubadili "glycogen" kuwa "glucose", glycogen ni kama jenereta, inatoa huduma pale chanzo kikuu cha nishati kinapozidiwa, pale nishati ya haraka inapohitajika aidha uko mazoezini au kiwango cha sukari kimeshuka, glycogen huvunjwa na kubadilishwa kuwa sukari (glucose), hivyo kuigilia kati kwa mchakato huu kunaongeza hatari ya kupata hypoglycemia. 

Hupunguza ufanisi wa insulini

Baadhi ya beta blockers mfano atenolol hupunguza ufanisi wa insulini, na hivyo kuongeza kiwango cha sukari kwenye damu na kufanya udhibiti wa kisukari kuwa mgumu zaidi. 

Huongeza uzito

Beta blocker kama metoprol zimehusishwa na na ongezeko la uzito kwa kasi ikiwa zimetumika muda mrefu. Hali hii ya uzito kuongozeka huongeza upinzani wa insulini (insulin resistance) na kufanya udhibiti wa Kisukari kuwa mgumu. 


DAWA ZA AFYA YA AKILI

Dawa kama olanzapine, clazapine na risperidone zinaweza kuchochea kwa kiasi kikubwa athari za ugonjwa wa kisukari. Hivyo kuchukua tahadhari na kutoa taarifa kamili kuhusu historia ya mgonjwa ni hatua muhimu. 

ANTIPSYCHOTIC

Jinsi dawa za afya ya akili zina athiri kisukari

Huongeza uzito

Olanzapine na Clozapine zinahusishwa na ongezeko kubwa la uzito aidha kwa kuongeza hamu ya chakula, ambapo mgonjwa atajikuta akila zaidi hasa vyakula vyenye sukari na mafuta mengi, au kupunguza shughuli za kimwili ambapo wagonjwa hukutana na hali za uchovu na usingizi, kupungua kwa shughuli za kimwili kunachochea ongezeko la uzito kwa sababu kiwango kidogo cha sukari kinatumika. Risperidone inaweza pia kuongeza uzito japo kwa kiasi kidogo, na kama tulivyoona awali ongezeko la uzito kupita kiasi kunaongeza upinzani wa insulini. 

Huongeza viwango vya sukari mwilini

Olanzapine na Clozapine pia zinahusishwa na nafasi kubwa ya kuongeza kiwango cha sukari mwilini, vilevile zinaongeza nafasi ya mtu asiye na kisukari kupata ugonjwa huo. Risperidone inaweza kuongeza kiwango cha sukari ingawa kwa kiwango kidogo. 

Huongeza kiwango cha lipidi

Olanzapine na Clozapine zinaweza kusababisha mabadiliko makubwa ya lipidi (cholesterol na triglyceride), na kuongeza hatari kwa wagonjwa wa kisukari kupata matatizo ya moyo na mishipa. 


BAADHI YA DAWA ZA MAUMIVU

Dawa kama Ibuprofen, Aspirin na Naproxen. Hizi ni dawa za kupunguza maumivu na uvimbe (NSAIDs), kwa wagonjwa wa kisukari dawa hizi zinaweza kuathiri viwango vya sukari ama kuathiri jinsi dawa za kisukari. 

picha ya dawa za maumivu zinazoathiri wagonjwa wa kisukari

Jinsi dawa za maumivu zinavyo athiri kisukari

Huathiri kazi ya figo

Ibuprofen, Naproxen na Aspirin zinaweza kudhoofisha kazi ya figo, jambo ambalo lina athiri jinsi dawa za kisukari zinavyoweza kutolewa mwilini na kusababisha madaliko yasiyo tabirika ya viwango vya sukari. 
Ufuatiliaji wa karibu sana unahitajika kwa wagonjwa wa kisukari wanao tumia dawa hizi. 

Hatari ya sukari ya kiwango cha chini (Hypoglycemia)

Dawa hizi zina hatari ya hypoglycemia (sukari ya kiwango cha chini) hasa pale zinapotumika na dawa za kisukari kama glipizide na insulini. Ufuatiliaji wa karibu wa viwango vya sukari na hali ya figo ni muhimu wakati wa kutumia dawa hizi. 

DAWA ZA KUPUNGUZA CHOLESTEROL

"Statins" kundi la dawa zinazotumika kupunguza viwango vya cholesterol, matumizi yake kwa wagonjwa wa kisukari huja na tahadhari, kwani zinaweza kuathiri viwango vya sukari mwilini na kuongeza hatari ya kupata kisukari.


Jinsi statins zinavyo athiri viwango vya sukari

Hudhoofisha utoaji na kuongeza upinzani wa insulini

Tafiti zimeonesha kuwa baadhi ya statins hasa kwenye dozi kubwa zinahusishwa na ongezeko dogo la hatari ya kupata kisukari anina ya 2, mfano Atorvastatin, Rosulvastatin na Simvastatin. 
Statins pia zinaweza kusababisha kuongezeka kidogo kwa viwango vya sukari ya kufunga (fasting blood glucose) na HbA1c (kipimo cha damu kinacho onesha wastani wa viwango vya sukari katika kipindi cha miezi miwili hadi mitatu)  ambavyo ni vipimo vya udhibiti wa sukari kwa muda mrefu. 

Hata hivyo mara nyingi faida za statins katika kupunguza hatari ya shambulio la  moyo na kiharusi hupita hatari hizi, hasa kwa wagonjwa walioko kwenye hatari kubwa ya magonjwa ya moyo, lakini ufuatiliaji wa mara kwa mara wa viwango vya sukari ni muhimu kwa wagonjwa wa kisukari walioko kwenye dozi kubwa za statins.  


Vitu vya kuzingatia kwa mgonjwa wa kisukari kabla ya kutumia dawa za magonjwa mengine

  • Usitumie dawa yoyote bila ushari wa daktari
  • Pima viwango vyako vya sukari mara kwa mara, angalau mara nne kwa siku au zaidi. 
  • Onana na daktari haraka ikiwa viwango vya sukari bado viko juu hata baada ya kutumia dawa zako za kisukari. 
  • Dhibiti ulaji wa vyakula vya wanga, na kufanya mazoezi kunasaidia kupunguza viwango vya sukari kwenye damu. 
  • Tembea na vitu vya dharura vya kusaidia kupandisha kiwango cha sukari mfano "glucose"

Comments

Popular posts from this blog

The Beauty Boosters

  Skin, Hair, and Nails – The Beauty Boosters When your skin is glowing, your nails are strong, and your hair is thick and healthy—you just feel better. But beauty isn’t just about what you apply on the outside. It starts from within. This article breaks down the top supplements that support hair growth, skin elasticity, nail strength, and that all-over glow. Why Do You Need These Supplements? Daily stress, age, poor diet, and harsh products can all affect your appearance. You might notice: Hair thinning or slow growth Dry, dull skin Brittle, weak nails Breakouts or premature aging Supplements can help fill the gaps in your diet and give your body the nutrients it needs to rebuild and repair. Collagen – The Beauty Glue Think of collagen as the “glue” that holds everything together. It’s a major part of your skin, muscles, bones, tendons, and ligaments—providing structure, support, and elasticity. So… You want to get rid of wrinkles? You want to strengthen your joints and bones...

DOMPERIDONE SYRUP: HATARI KWA WATOTO CHINI YA MIAKA 12!

Unapofika duka la dawa kuulizia dawa ya kuzuia kutapika kwa mtoto wako, kuwa makini! Sio kila dawa ya mfumo wa kimiminika (syrup) inafaa kwa mtoto, HAPANA.  Dawa hii inaweza kusababisha madhara makubwa kwa mtoto wako, na tuwe wakweli tu, kuna watu wako kwenye hizi "pharmacy" zetu, hawajali kabisa na pengine hawajui dawa ipi ni salama kwa mtoto ama la!  Hakikisha unasoma karatasi ya maelezo iliyopo ndani ya boksi la dawa kwa uhakiki na ufahamu zaidi. Tutumie msemo wa kimombo unasema "Better safe than sorry" Haya ni baadhi ya madhara yanayoweza kusababishwa na dawa hii:  Hatari kubwa kwa MOYO Domperidone inaweza kuathiri mfumo wa umeme wa moyo na kuongeza muda wa QT ( QT prolongation ). Hii inaweza kusababisha mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida (arrythmia), hali ya hatari inayoweza kutishia maisha isipo dhibitiwa haraka.  Matatizo ya mfumo wa fahamu Domperidone hufanya kazi kwa kuongeza kasi ya utumbo na kuzuia kemikali fulani kwenye ubongo (dopamine antagonist). Ingawa...